UN:Pawepo mpango endelevu wa kurejea kwa wakimbizi wa Syria
24 Januari 2025Akizungumza katika ziara yake nchini Lebanon, baada ya kukutana na Rais Joseph Aoun wa nchi hiyo, Grandi alisema ziara hiyo ni sehemu ya ziara ya kikanda ya kutafuta njia bora za kuwasaidia wakimbizi wa Syria wanaorejea nchini mwao.
Grandi ameongeza kuwa wanataka kuhakikisha kwamba mchakato wa kurejea kwa wakimbizi hao ni endelevu, na kwamba kuna haja ya kuimarishwa kwa usalama na utulivu wa kisiasa, kuheshimiwa kwa haki za jamii zote nchini Syria, pamoja na uungaji mkono wa jumuiya ya kimataifa kwa ajili ya kujenga upya nchi ambayo imeharibiwa na miaka kadhaa ya vita.
Ulaya, Arabuni wakutana kuijadili Syria
Mkuu huyo, pia alipongeza kuwepo kwa matumaini kwa eneo hilo kufuatia kuanguka kwa Assad, akisema kumefungua njia ya kutatua mzozo wa muda mrefu wa kibinadamu.
UNHCR inasema zaidi ya wakimbizi 200,000 wa Syria wamerejea makwao tangu kuondolewa kwa Assad mapema mwezi Desemba.