MigogoroMashariki ya Kati
UN: Makubaliano ya usitishwaji mapigano Gaza yaheshimiwe
1 Machi 2025Matangazo
Wito wa Guterres umetolewa wakati awamu ya kwanza iliyoanza kutekelezwa Januari 19, inatarajiwa kumalizika leo Jumamosi, lakini masharti yake yanatarajiwa kudumishwa wakati huu mazungumzo ya kuelekea awamu ya pili yakiendelea.
Soma pia: UN: Hali ya Gaza ni ya kutisha na ni janga kubwa
Kulingana na taarifa ya shirika la habari la Ujerumani dpa, kundi la Hamas limekataa pendekezo la Israel la kurefusha kwa siku 42 awamu hii ya kwanza ya usitishwaji mapigano, ikitaka kuelekea moja kwa moja kwenye awamu ya pili inayokusudia kusitisha kabisa vita hivyo,huku Hamas ikiwaachilia mateka waliosalia na wanajeshi wa Israel wakikamilisha zoezi la kuwaondoa wanajeshi wao huko Gaza.