UM: Kupunguzwa misaada kunatishia maisha ya watoto
25 Machi 2025Matangazo
Fouzia Shafique, mkurugenzi mshiriki wa Shirika la kimataifa la kuwahudumia watoto UNICEF, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba jumuiya ya afya duniani ina wasiwasi mkubwa kuhusu hali ilivyo.
Ripoti ya shirika hilo, imeonya kuwa athari ya kukatizwa kwa pesa za msaada itakuwa mbaya katika mataifa ambapo viwango vya vifo vya watoto wachanga tayari ni vya juu mno, kama vile katika Kusini mwa Jangwa la Sahara na kusini mwa Asia.
Katika taarifa, mkuu wa shirika hilo la UNICEF Catherine Russell, amesema kupunguza vifo vya watoto vinavyoweza kuzuilika ni mafanikio makubwa lakini akaongeza kuwa bila kuwepo kwa sera sahihi na uwekezaji wa kutosha, kunahatarisha kurudi nyuma kwa hatua za ufanisi zilizopigwa.