MigogoroUlaya
Ukraine: Urusi imefanya mashambulizi licha ya agizo la Putin
8 Mei 2025Matangazo
Serikali ya Kiev imesema pia kuwa hapakuwepo na mashambulizi ya makombora au droni yaliyoripotiwa Alhamisi asubuhi.
Agizo la Rais wa Urusi Vladimir Putin la kusitisha mapigano nchini Ukraine kwa muda wa siku tatu limeanza kutekelezwa kuanzia leo asubuhi ili kwenda sambamba na siku ya kuadhimisha miaka 80 ya ushindi dhidi ya manazi wa Ujerumani wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia.
Kesho Ijumaa, kutashuhudiwa gwaride mjini Moscow ambako viongozi mbalimbali ikiwa ni pamoja na rais wa China Xi Jinping wameanza kuwasili ili kushiriki sherehe hizo zinazofahamika kama "Siku ya Ushindi."