Ujumbe wa Hamas waelekea Cairo kwa mazungumzo kuhusu Gaza
22 Aprili 2025Matangazo
Afisa wa kundi hilo la Hamas, amesema kuwa ujumbe huo utakutana na maafisa wa Misri kujadili mipango hiyo mapya na kuongeza kuwa timu hiyo itamjumuisha afisa wa ngazi za juu wa Hamas, Khalil Al-Hayya.
Hamas wahimizwa wakubali mkataba ili misaada iingie Gaza
Mazungumzo ya sasa yanafanyika siku moja baada ya balozi mpya wa Marekani nchini Israel, Mike Huckabee, kuitaka Hamas kukubali makubaliano ya Israel ya kuwaachia huru mateka ambao bado wanashikiliwa katika Ukanda wa Gaza ili kuwezesha kuingizwa kwa misaada ya kibinadamu katika ukanda huo.