UhalifuUjerumani
Ujerumani yalipiga marufuku kundi la itikadi kali
13 Mei 2025Matangazo
Miongoni mwa waliokamatwa ni Peter Fitzek ambaye ndiye aliliunda kundi hilo na kisha kujitangaza kuwa "Mfalme", mnamo mwaka mwaka 2012.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ujerumani imesema kundi hilo ni sehemu ya mtandao mpana wa vuguvugu la itikadi kali za mrengo wa kulia linalofahamika kama "Reichsbürger" ambalo linapinga uhalali wa jamhuri ya sasa ya Ujerumani.
Wizara hiyo imesema kwa zaidi ya miaka 10 kundi hilo limeunda na kuendesha taasisi zinazofanana na serikali, likichapisha sarafu yake yenyewe, kutoa vitambulisho na hata bima kwa wanachama wake wanaofikia 6,000.